May 20, 2016

WEMA SEPETU AMWAGIA SIFA KEDEKEDE ALIKIBA BAADA YA WIMBO WA "AJE" NA DILI HILI JIPYA LA KIBA

Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa msanii Alikiba ni mtu wa kumuacha kutokana na uwezo wake wa kuimba na namna a... thumbnail 1 summary
Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa msanii Alikiba ni mtu wa kumuacha kutokana na uwezo wake wa kuimba na namna ambavyo anaweza kuipangilia sauti yake kwenye muziki.
Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote

"Ila huyu bichwa wangu mimi ananikoshaga sana. Na mumuachage tu kwakweli. Bichwa una sifa lakini maana si kwa Vocal hizi. Halafu mimi siwezi kukubania namba bana. Naupenda sana huu wimbo jamani. Wajua kutukunaga mashabiki wako. Good work Bichwa wangu Officialalikiba did it again ladiez & Gentlemen"aliandika Wema Sepetu 

Mbali na hilo Wema Sepetu amempa pongezi msanii Alikiba kwa kuweza kusaini mkataba chini ya kampuni ya muziki ya 'Sony Music' na kusema kuwa alistahili hilo na zaidi ya hilo kwani anakipaji kikubwa.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments