Hizi ndizo za sababu za Rais Magufuli kufuta sherehe za Uhuru mwaka janaRais Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika maadhimisho ya sherehe za miaka 55 ya uhuru, Ijumaa hii aliwaeleza Watanzania sababu zilizomfanya kufuta maadhimisho ya miaka 54 ya uhuru wa Tanzania bara mwaka jana.
Rais Magufuli alifanya kitu cha tofauti na Marais waliopita, na jana aliweza kutoa sababu za kusitisha sherehe hiyo mwaka huo.
“Kwanza inabidi sherehe za mwaka jana tuziazimishe kama zilivyopangwa kwasababu hii,sababu ya kwanza sherehe zenyewe zilitakiwa zifanyike baada ya mwezi mmoja kuapishwa kwahiyo hata baraza langu na watendaji wengine nilikuwa bado sijawateua. Lakini sababu ya pili nilipoambiwa gharama za sherehe hizo mwaka jana zilikuwa bilioni nne nikawa najiuliza bilioni 4 kuna mambo yapi yatakayofanyika?” alisema Magufuli.
“Itakuwa ni kualika wageni, watakula chakula,patakuwa na posho na na kadhalika. Nilipouliza hizo posho na chakula watakula Watanzania wote, wakasema ni wale wachache tu watakaokuwa wamealikwa na ndiyo maana nikaamua hizo bilioni nne ziende kupanua barabara za Ali Hassani Mwinyi ambayo inapitiwa na Watanzania wote,” aliongeza.