Sio Kila EX wako anayeomba Mrudiane anamaanisha! Wengine huomba kurudi ili wakutesti tu jinsi ulivyo Mbulula,jinsi usivyo na msimamo na jinsi ulivyo CHEAP na huna Misimamo wala
Kipaji cha Raymond kilianza kuonekana mwaka 2011 baada ya kushiriki kwenye mashindano ya kuchana yaani (FreeStyle) mkoani Mbeya na kuwa mshindi wa kwanza,alipokuja Dar kwenye fainali za mashindano hayo akaibuka pia kuwa mshindi ndipo Tip Top Connection ilipomchukua na kuwa chini yake.
Raymond ameshaoneka na kwenye majukwaa mengi hasa kwenye show zaMadee,Kutokana na ukaribu wa Label ya TipTop Connection na WCB,Menejimenti zimekaa chini na kukubaliana kumtoa kupitia label ya Wasafi (WCB) ambayo uongozi wa label hiyo upo chini ya Diamond Platnumz.
Najua nina watu wangu ambao mlikuwa na hamu ya kufahamu vitu vingi kutoka kwa msanii huyo mpya kutoka WCB, sasa basi tazama hii video hapa chini Raymond akielezea alivyokutana na Diamond mpaka kusainiwa katika label ya WCB (Wasafi).