May 20, 2016

Ben Pol: Najiogopa Nikivaa Hereni na Kuchora Tatoo, Hivi Kwangu Ni HAPANA

Ben Pol ni mmoja kati ya wasanii wachache kwenye muziki wa Bongo Fleva wasiokuwa na makuu. ‘Moyo Mashine’ ni moja kati ya nyimbo zinazo... thumbnail 1 summary
Ben Pol ni mmoja kati ya wasanii wachache kwenye muziki wa Bongo Fleva wasiokuwa na makuu.
‘Moyo Mashine’ ni moja kati ya nyimbo zinazofanya vizuri kwenye TV na redio na kufanikiwa kuweka rekodi ya kuwa na views nyingi kwa muda mfupi kuzidi nyimbo nyingine ambazo Ben Pol amewahi kuziachia.

Akiongea kwenye kipindi cha Clouds 360, kinachoruka kupitia Clouds TV, Ben Pol amesema, “najiogopa, nawaza hivi itakuwaje nikivaa hereni au kuchora matatoo.”

“Wazazi hawatasumbua, kwa umri wangu huu naweza kufanya kitu chochote. Lakini mimi mwenyewe naona hivi itakuwaje, labda naenda kama benki hivi. Nataka kufocus kwenye muziki mzuri na ubunifu kwenye muziki lakini zile mbwembwe hapana,” aliongeza.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments