May 13, 2016

MAPAMBANO YA RONALDO NA MESSI HADI KWENYE MSHIKO

Ni Cristiano Ronaldo aliyezaliwa February 5, 1985 huko Santo António jijini Lisbon Ureno, Huyu ni fundi sana wa uwekezaji ukiachana na uw... thumbnail 1 summary
Ni Cristiano Ronaldo aliyezaliwa February 5, 1985 huko Santo António jijini Lisbon Ureno, Huyu ni fundi sana wa uwekezaji ukiachana na uwezo wake wa kuutendea haki mchezo wa soka. Kwasasa Ronaldo anafanya kazi na makampuni
makubwa duniani kama Nike, Emporio Armani , KFC , Coca Cola na kampuni ya mafuta ya Castrol.

Makumpuni yote jumla yanamwingizia kiasi cha $28 million. Huku Nike pekee ikimwingizia kiasi cha $14.1 million, wakati kwa mwaka anatengeneza jumla ya kiasi cha $82.1 million, hivyo anakila haki ya kuongoza kwenye orodha ya wanamichezo wanaoingiza mkwanja mrefu.

Lionel Messi amezaliwa June 24, 1987 Rosario, Argentina , mkataba wake mnono ni kutoka kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas unamwingizi kiasi cha $13 Million kwa mwaka wakati huo akifanya kazi na makampuni ya Pepsi, Audemars, Piguet ,Dolce,Gabanna,Ea Sports,Herbalife /Turkish Airlines, Proctor na Gamble. Makapmuni haya yanamfanya aingize kiasi cha $21.3 kwa mwaka. Huku jumla ya mapato yake yakifikia $76.5 million kwa mwaka na kumfanya akae kwenye nafasi ya pili.

Zlatan Ibrahimovic mchezaji mwenye msimamo akiwa amezaliwa October 3, 1981, huko Malmö, Sweden. Anafanya kazi na makampuni mbalimbali ikiwemo kampuni yake binafsi ya kutengeneza pafyumu, lakini pia anamkataba na kampuni ya Nike na anaingiza kiasi cha $9 million kwa mwaka huku pia akipokea mshahara wa Euro 18 million kwa mwaka. Jumla ya mapato yake kwa mwaka ni $37.3.

Chini ndio jedwali la wacheza kadanda 10 waliovuna pesa ndefu mwaka 2015 kwa mjibu wa Forbes.


No Comments Yet.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments