April 21, 2016

KWA MUJIBU WA JARIDA LA GQ, HAWA NDIO MASTAA WANAONYUKA ‘PAMBA’ ZAIDI DUNIANI.

Kwa mujibu wa Jarida maarufu la GQ, marapa Future na Drake ndio imewataja kama mastaa wanaopiga pamba zaidi Duniani. thumbnail 1 summary
Kwa mujibu wa Jarida maarufu la GQ, marapa Future na Drake ndio imewataja kama mastaa wanaopiga pamba zaidi Duniani.

Future ametajwa kuwa mkali wa kofia za BRIM “Lord of the Brim” na wote wametokea kwenye kava za jarida hili.

Kwenye orodha hii pia wapo Odell Beckham Jr, Aziz Ansari, Diplo, na Ryan Reynolds.

Pia Ikiwa imebaki wiki mbili mpaka kutoka kwa album yake Drake amefungua duka la Views From the 6, mjini New York likiwa limedhaminiwa na Beats by Dre.

Watu zaidi ya 800 walisimama mstari kununua bidha za Views wakati duka linafunguliwa.

Album inatoka April 29 na nyimbo kubwa kwa sasa kutoka kwenye cd hii ni pamoja na “One Dance” Ft WizKid na “Pop Style” Ft Jay Z na Kanye West.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments