August 28, 2014

Umeisoma ripoti ya leo kuhusu chai na chakula kwenye bunge la katiba?

Gazeti la Mtanzania August 28 2014 ndio limeripoti hii stori kuhusu Bunge la Katiba linaloendelea Dodoma, kikubwa ni gharama mbalimbali z... thumbnail 1 summary
Screen Shot 2014-08-28 at 10.20.29 AMGazeti la Mtanzania August 28 2014 ndio limeripoti hii stori kuhusu Bunge la Katiba linaloendelea Dodoma, kikubwa ni gharama mbalimbali zinazotumiwa na
Wajumbe.
Wameandika bunge la katiba lateketeza mamilioni ya fedha ambapo kikombe cha chai na biskuti au karanga kinalipiwa shilingi elfu 10 kila siku kwa kila Mjumbe mmoja licha ya kwamba kila Mjumbe anapokea posho ya siku ambayo ni laki mbili na elfu 30.
Kwenye sentensi ya pili wameandika, chakula cha mchana kila Mjumbe analipiwa elfu 16 kwa siku ambapo kwa siku hiyohiyo iendayo kwa Mungu, ni shilingi milioni 8 hulipwa kama gharama za ukumbi wa kufanyia mikutano.
Una chochote cha kusema kutokana na hili?

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: