August 26, 2014

MASHABIKI WAMUUA MCHEZAJI ALGERIA

MCHEZAJI kutoka Cameroon amekufa baada ya kupigwa kichwani wakati thumbnail 1 summary
MCHEZAJI kutoka Cameroon amekufa baada ya kupigwa kichwani wakati
mashabiki waliokereka waliporusha mawe mwisho wa mechi ya Ligi ya Algeria.
Albert Ebosse enzi za uhai wake.
Albert Ebosse, aliyekuwa na umri wa miaka 24, ndiye aliyefunga mabao mengi katika Ligi ya Algeria msimu uliopita.
Alirushiwa kitu wakati mashabiki walipokerwa kuwa timu yake, JS Kabylie, iliposhindwa kwa mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa nyumbani, Tizi Ouzou.

Marehemu ndiye aliyefunga bao hilo pekee kwa timu yake.
Wizara ya mambo ya nchi ya Algeria imeamrisha uchunguzi ufanywe kuhusiana na kifo hicho.GPL (P.T)

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: