May 19, 2016

Drake amfunika vibaya Justin Bieber kwenye mtandao wa Spotify

Drake ambaye hivi karibuni ametoa album yake mpya ya VIEWS iliyogonga platinum ndani ya wiki moja na kuanza kuuzwa kwenye mitandao tofauti,... thumbnail 1 summary
Drake ambaye hivi karibuni ametoa album yake mpya ya VIEWS iliyogonga platinum ndani ya wiki moja na kuanza kuuzwa kwenye mitandao tofauti, imeweka rekodi mpya.

Drake kwa sasa ametajwa kuwa msanii aliyesikilizwa mara nyingi zaidi kwenye mtandao wa Spotify na kumpiku staa wa pop Justin Bieber. Drizzy amempoteza Justin Bieber kwa kusikilizwa na watu zaidi ya milioni 10 kuliko Justin.

Drake ana watu 3,185,045,281 na Justin ni watu 3,175,636,461. Wasanii wengine ambao wapo kwenye orodha hii ni pamoja na The Weeknd ,Rihanna , Fetty Wap na Nicki Minaj.

Nafasi hii Drake alishika mwaka 2015 na album yake ya If You’re Reading This It’s Too Late.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments