Liverpool imepangwa kundi moja na mahasimu Manchester United katika hatua ya 16 ya Ligi ya Ulaya (Europa League).
Timu zote hazipo katika nne bora Ligi Kuu, ushindi wa shindano hilo utakuwa njia nzuri kwa wao kufudhu msimu ujao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Timu hizo zitacheza mara mbili ndani ya siku saba, mechi ya kwanza itachezwa Anfield Machi 10 na marudio yatakuwa Old Trafford Machi 17.
LIVERPOOL V MANCHESTER UNITED
Kucheza: 177
Liverpool ushidni: 60 (33.9%)
United ushindi: 72 (40.7%)
Sare: 45 (25.4%)
Magoli: 244-228
Mechi nyingine hatua ya 16 Europa League ni;
Shakhtar Donetsk v Anderlecht
Basel v Sevilla
Villarreal v Bayer Leverkusen
Athletic Bilbao v Valencia
Liverpool v Manchester United
Sparta Prague v Lazio
Borussia Dortmund v Tottenham
Fenerbahce v Braga