Unamjua yule Papaa Misifa aliyekuwa meneja wa mwanamuziki Rich Mavoko? Kama jibu ni ndiyo basi ametoa kali ya mwaka kwa kudai kuwa, eti Mavoko hawezi kutusua kimuziki kwa kuwa amempa laana.
Haya hapa maneno ya Papaa Misifa:
“Yaani Mavoko ana laana yangu, nakwambia mimi msanii akiondoka kwa kuvunja mkataba kwangu kamwe hataendelea kwani huwa nina laana mbaya, Mavoko nimemlaani mpaka atakaponilipa mkwanja wangu ninaomdai kama milioni 100 hivi kwa sababu alivunja mkataba kwangu.”