February 26, 2016

Baraka Da Prince Ngoma Ambayo Inafuta Nimefanya na Ali Kiba.

Msanii wa bongo fleva Baraka da Prince ambaye saivi anafanya vizuri na wimbo wa “Siwezi” ameweka wazi kuwa pengine baada ya wimbo wake hu... thumbnail 1 summary
Msanii wa bongo fleva Baraka da Prince ambaye saivi anafanya vizuri na wimbo wa “Siwezi” ameweka wazi kuwa pengine baada ya wimbo wake huo wa sasa huenda akatoa ngoma ambayo amefanya na Ali Kiba.
Baraka amesema kuwa yeye ni mshabiki mkubwa wa kazi za Ali Kiba ukiachana na ukweli kwamba yeye na Kiba ni kama mtu na mdogo wake kimuziki.
Kupitia Redio One Baraka alisema “mimi ni mshabiki mkubwa sana wa Kiba,napenda kazi zake..nilihisi kama nahitaji kufanya nyimbo na mtu na nikamfikiria jamaa mwenyewe awe Kiba,nilipoongea akaitikia poa akaniambia kuna utaratibu niufuate kwa kuwa yeye yupo chini ya menejimenti,nikafata utaratibu tukaingia studio tukawa tumepiga kitu” alifunga Baraka na kuongeza ngoma hiyo itatoka hivi punde.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: