Rais John Pombe Magufuli |
Kaimu Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Katavi, Christopher Nakua alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Januari 18, mwaka huu katika eneo la Mtaa wa Kawajense baada ya kuandaliwa mtego ambao ulifanikisha kukamatwa kwake.
Alisema mtuhumiwa alikamatwa kufuatia Ofisi ya Takukuru kupokea taarifa kutoka kwa mlalamikaji kuwa Ofisa Mtendaji huyo anamuomba rushwa kiasi cha Sh 30,000 ili asimpeleke kwenye Baraza la Kata kwa kosa la kufungua sehemu yake ya biashara wakati ni muda wa kufanya usafi na kutokushiriki kufanya usafi.
Ilidaiwa kuwa baada ya kupokea taarifa hizo ofisi ya Takukuru ilifanya uchunguzi na baada ya kuridhika na maneno ya mlalamikaji ndipo mtego ulipoandaliwa na mtuhumiwa kukamatwa.
Kamanda Nakua alisema mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa tuhuma zinazomkabili ambazo ni kuomba rushwa ya fedha taslimu Sh 30,000, shtaka la pili litakuwa ni kupokea rushwa ya Sh 30,000 kinyume cha kifungu cha 15 (1) (a) cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa Na 11 ya mwaka 2007.