May 16, 2016

Mchezo wa Manchester United dhidi Bournemouth umesogezwa mbele kwa sababu za kiusalama

Mechi ya mwisho ya Ligi Kuu ya Uingereza kati ya Manchester United na Bournemouth umehairishwa kufuatia kubainika kwa kifurushi kinachoti... thumbnail 1 summary
Mechi ya mwisho ya Ligi Kuu ya Uingereza kati ya Manchester United na Bournemouth umehairishwa kufuatia kubainika kwa kifurushi kinachotiliwa shaka katika dimba la Old Trafford.


Mashabiki katika majukwaa mawili ya Sir Alex Ferguson na Stretford End, waliondolewa kabla ya kuanza kwa mchezo huo na mbwa wa kunusa milipuko waliletwa ili kusaidia kubaini kifurushi hicho.


Awali nchezo huo ulicheleweshwa kuanza na kisha muda mfupi baadae mechi hiyo ilihairishwa kabisa kufuatia ushauri uliotolewa na polisi. Maafisa usalama walisimamia zoezi la mashabiki kutoka nje ya uwanja.


Baada ya kuahirishwa kwa mchezo huo ratiba ya lini utachezwa mchezo huo imetajwa kuwa ni Jumanne ya May 17 2016.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments