February 23, 2016

Gigy Money Afunguka "Hemedy PHD Aliwahi kugombana na Rich Mavoko Kwa Ajili Yangu"

Video queen Gigy Money amefunguka kwa kudai kuwa aliwai kutoka kimapenzi na Hemedy PHD na Rich Mavoko. Akiongea katika kipindi cha Planet... thumbnail 1 summary
Video queen Gigy Money amefunguka kwa kudai kuwa aliwai kutoka kimapenzi na Hemedy PHD na Rich Mavoko.
Akiongea katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Television, Gigy alisema aliamini wasanii hao wangeweza kumtoa kimaisha lakini wanaishia kumcheza na kumuacha.

“Mimi nilishawahi kudate na Hemed PHD nikiamni atanitoa nitatoboa, lakini wapi. Hemedi alishawahi kugombana na Rich Mavoko kwa ajili yangu, tena kipindi hiko niko form two, unajua maisha kila mtu kuna aliyopitia,” alisema Gigy.

“Nilishawahi kuwa na mtu ambaye hata hatuendani lakini nilikuwa nalazimika, mtu ameshanimilikisha gari, nyumba, tukitoka nalazimika kuvaa angalau nifanane nae kiutu uzima”, aliongeza Gigy.

Gigy ambaye amecheza vitendo kwenye video mpya ya Godzilla ‘Get High’, hivi karibuni alikuwa kwenye vichwa vya habari za burudani baada ya kudai ametoka kimapenzi na msanii Tekno Miles kutoka Nigeria.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: