April 30, 2015

Diamond, Ali Kiba wachuana Tuzo za Watu

WANAMUZIKI mahiri wa muziki wa Bongo fleva nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ na Ali Kiba, ni miongoni mwa wasanii wanaochuan... thumbnail 1 summary



WANAMUZIKI mahiri wa muziki wa Bongo fleva nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ na Ali Kiba, ni miongoni mwa wasanii wanaochuana katika Tuzo ya Msanii Bora wa Kiume katika Tuzo za Watu 2015.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Bongo 5 Media Group, inayoratibu tuzo hizo, Nancy Sumari, wasanii wengine walio katika kipengele hicho ni Elias Barnaba, Ommy Dimpoz na Jux.

Katika kipengele cha msanii bora wa kike wanaochuana ni Lady Jaydee, Linah, Mwasiti, Shilole na Vanessa Mdee.

Filamu ya Chausiku, Kigodoro, Madam, Mshale wa Kifo na Sunshine zinashindana kwenye kipengele cha filamu zinazopendwa.

Msanii JB na Ray, wanachuana katika kipengele cha mwongozaji bora wa filamu sambamba na Leah Mwendamseke, Timothy Conrad na William Mtitu.

Alisema Jumamosi yatatangazwa majina ya tano bora na Mei 8 mwaka huu yatatangazwa majina ya waliotinga tatu bora ambapo fainali itafanyika Mei 22.

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: