March 25, 2016

Linah Sanga Amewahi Kutoa Rushwa ya Ngono ? Ipo Hapa

Tetesi zimezidi kuvuma na zimekwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa wasanii wa kike wale wakali bongo ili waweze kufanya video nzuri na waon... thumbnail 1 summary
Tetesi zimezidi kuvuma na zimekwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa wasanii wa kike wale wakali bongo ili waweze kufanya video nzuri na waongozaji wakubwa zaidi pia wanatoa rushwa
hiyo ya ngono.

Kipindi cha Enews kinachorushwa na East Africa Television kilitaka kufahamu kama kuna ukweli wasanii hao wa kike huhonga ngono ili wafanyiwe kazi nzuri kwenye hizo kampuni kubwa, Linah Sanga ambaye hata yeye amefanikiwa kufanya videos na waongozaji wakubwa wa video barani Afrika akiwepo Godfather alikuwa na haya ya kusema.

"Sijui kama ipo hivyo sababu mimi kama msanii wa kike sijawahi kufanya kitu kama hicho, kwa hiyo sidhani kama hicho kitu ni cha kweli kwa sababu ukifuatilia kwa wasanii wakubwa wa

kike ambao tumeweza kufanya kazi na madirectors wakubwa kama God Father na wengine ni mimi, Vanessa, labda na Aika kwa sasa hivi ambao tayari tumeshatoa kazi zetu, kwa hiyo sidhani kama hicho kitu ni kweli kwa sababu tunafanya kazi na kazi zinalipa ndiyo maana tunaweza kufanya kazi na watayarishaji wakubwa kama hivyo". Alisema Linah Sanga.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments