Maandamano yaliyofanywa katika jimbo hilo.Meya wa Mji wa Baltimore nchini Marekani, Stephanie Rawlings-Blake, amesema kuwa amehudhunishwa na kuvunjwa moyo baada ya polisi sita kushtakiwa, kufuatia kifo cha mwananaume mweusi, Freddie Gray.Polisi mmoja anakabiliwa na mashtaka ya mauaji huku wengine watano wakikabiliwa na mashtaka ya kuua bila kukusudia.
Tangazo hilo lilisababisha watu kusherehekea kwenye mji wa Baltimore lakini wengine waliiendelea kuandamana.Wakili anayewakilisha chama cha polisi katika mji huo, alilaani kile alichokitaja kuwa kuharakisha katika kuwafungulia mashtaka polisi hao.
Rais wa Marekani Barack Obama anasema kuwa, ni muhimu uchunguzi wa kina ukafanyika ili kubainisha ukweli kuhusu kile kilichosababisha kifo cha Bw. Gray.
CHANZO: BBC