July 02, 2014

HALI TETE RAY NA JOHARA KUGAWANA KILA KITU HADI......

Hali katika kampini ya RJ inayoongozwa kwa ubiya kati ya Vicent Kigosi ( Ray) na Blandina Chagula ‘Johari’, inazidi kuwa tete kwa kile... thumbnail 1 summary

ray
Hali katika kampini ya RJ inayoongozwa kwa ubiya kati ya Vicent Kigosi ( Ray) na Blandina Chagula ‘Johari’, inazidi kuwa tete kwa kile kinachoelezwa kuwa johari hataki kufanya kazi pamoja na ‘mke mwenza’  Chuchu Hans.
Chanzo hicho ambacho kipo karibu na wasanii hao kilisema kuwa mwezi mmoja uliopita Johari na Chuchu, walikuwa katika kuelekea kuelewana ambapo johari, alishakubali yaishe kuwa Ray wake ameshapokonywa na mtoto huyo wa Kitanga .
Mnyetishaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya Johari kuwa katika hali hiyo,ndipo Chuchu alipoanza kutanua makucha yake ndani ya kampuni kwa kujifanya ni mmoja kati ya wakurugenzi wakati ukweli haupo hivyo.
Chanzo hicho kilizidi kusema kuwa imefikia hatua Chuchu, kaanza kutoa amri kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo bila ya kupata kibali kutoka kwa wakurugenzi waasisi ambao mtaji wao unadaiwa kutokana na  Johari ‘kumpiga’ changa la macho mfanyabiashara maarufu kutoka mkoani Mbeya.
Mpashaji huyo alizidi kusema kuwa bifu liliibuka upya mkoani Dodoma, ambako Ray na Johari walikwenda katika ziara ya Kilimanjaro Music Awards Tour, na mashabiki wao kuwataka wapande jukwaani kwa pamoja.
Mtoa habari hiyo alisema kuwa kuwa kutokana na hali hiyo, ndipo Chuchu alipoanzisha bifu la chinichini lililopelekea hadi sasa kwenye kampuni hiyo kuzuka mtafaruku mkubwa huku Johari, akitaka kujitenga kabisa na Ray lakini kinachomkwamisha ni pesa zake nyingi alizowekeza.
Inadaiwa  kuwa Johari amekuwa mkali sana sasa hivi akimtaka mkurugenzi mwenzake Ray, wagawane kila kitu mpaka nguo za ndani walizonunua kwa pesa za kampuni yao hiyo.
Katika kufuatilia habari hizo ili kupata ukweli kuhusiana na timbwili hili mwanahabari wetu aliwasaka wote kwenye simu zao za mkononi, lakini wote hawakutaka kutoa ushirikiano kwa kile walichokieleza kuwa wapo bize na maswala binafsi.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: