February 16, 2016

Kanye West aomba pesa kutoka kwa mmiliki wa "Facebok" Zuckerberg

Mwanamuziki Kanye West amemuomba hadharani mwaanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg ampe usaidizi wa kifedha. thumbnail 1 summary
Mwanamuziki Kanye West amemuomba hadharani mwaanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg ampe usaidizi wa kifedha.

West anataka Zuckerberg awekeze $1bn (£700m) katika miradi yake akisema yeye binafsi hana “rasilimali za kutosha” kuunda kile ambacho “anaweza”.

Ametoa ombi hilo siku chache tu baada ya kutangaza kwamba ana deni la $53m (£36m) alipokuwa akitoa albamu yake mpya.

West alijitetea kupitia msururu wa jumbe kwenye Twitter.

Waandishi wa BBC Newsbeat wamewasiliana na maafisa wa Facebook ambao wamesema: “Hatuna lolote la kusema kwa sasa.”

Jambo la kushangaza ni kwamba Kanye West amemuomba Zuckerberg usaidizi kupitia Twitter ambao ni mtandao unaoshindana na Facebook.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: