February 17, 2016

Chelsea yapokea kipigo dhidi ya PSG, lakini wamevunja rekodi hii ya PSG

Hatua ya 16 bora ya michuano ya Klabu Bingwa Ulaya imechezwa usiku wa February 16 kwa michezo miwili kupigwa katika viwanja vya  Pa... thumbnail 1 summary

Hatua ya 16 bora ya michuano ya Klabu Bingwa Ulaya imechezwa usiku wa February 16 kwa michezo miwili kupigwa katika viwanja vya Parc des Princes na Estádio da Luz, michezo miwili iliyopigwa usiku huo ni mchezo, kati ya Benfica dhidi
ya Zenit St. Petersburg na mchezo wa PSG dhidi ya Chelsea.
3983
Mchezo kati ya Chelsea dhidi ya PSG, ndio ulikuwa unatajwa kuwa mchezo wenye mvuto zaidi, kwani klabu ya PSG haikuwa na rekodi nzuri katika mechi zao sita, walizowahi kukutana, Chelsea alikuwa kashinda mara mbili, na kufungwa mara moja sare ikiwa ni michezo mitatu. Lakini PSG walikuwa na rekodi ya kutokufungwa katika mechi zake 34 msimu huu ilizocheza katika mashindano.
3506
PSG wamefanikiwa kubebwa na takwimu yao ya kutofungwa msimu huu, kwani wamefanikiwa kuiadhibu Chelsea kwa jumla ya goli 2-1, magoli ya PSG yalifungwa naZlatan Ibrahimovic dakika ya 19 na Edinson Cavani dakika ya 78, wakati Chelseawalifunga goli la kufutia machozi dakika ya 45 kupitia kwa mnigeria John Obi Mikel, goli la Chelsea limevunja rekodi ya PSG ya kutofungwa goli hata moja katika michuano yaUEFA msimu huu katika dimba lake la nyumbani.
Matokeo ya mechi nyingine
  • Benfica 1 – 0 Zenit St. Petersburg
Video ya magoli ya mechi ya PSG Vs Chelsea

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: