May 07, 2015

Nilipofukuzwa CHADEMA nilitamani kujiunga na Chama cha NCCR Mageuzi

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa alipofukuzwa wanachama katika chama cha Demokrasia na Maendeleo... thumbnail 1 summary
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa alipofukuzwa wanachama katika chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alitamani kujiunga na Chama Cha NCCR-Mageuzi kwani ndicho chama ambacho kilikuwa kinaendana na itikadi yake anayoifuata na kuiamini ambayo ni itikadi ya Ujamaa. Zitto Kabwe amefunguka haya leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa facebook wa EATV katika kipengele cha KIKAANGONI ambacho kimeanza upya katika msimu wa pili na kitakuwa kikifanyika kila Jumatano kuanzia saa nane mchana mpaka kumi Alasiri.
Zitto Kabwe alisema kuwa alishindwa kujiunga na Chama hicho cha NCCR-Mageuzi kutokana na kuwepo kwa matatizo hivyo aliona siyo vyema kujiunga nacho, ndiyo maana alifikiri kuwa na chama cha siasa ambacho kitakuwa na misingi na itikadi ambayo yeye anaiamini na kuisimamia.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: