March 31, 2015

MWANAMKE MSAGAJI ANAOMBA NIMPE UJAUZITO ILI AZAE MTOTO...USHAURI JAMANI NIFANYEJE...??

Kuna dada mmoja nje ya nchi ambaye anataka kuja hadi hapa Sikonge ili  nimtungishe Mimba na hatimaye azae mtoto. Huyu mdada ni... thumbnail 1 summary



Kuna dada mmoja nje ya nchi ambaye anataka kuja hadi hapa Sikonge ili 

nimtungishe Mimba na hatimaye azae mtoto. Huyu mdada ni mtu ambaye ninafahamiana naye kwa miaka
mingi kidogo tangu nikiishi nje ya nchi ambapo siku hizo, hakuwa au nilikuwa sijajua kama ni Msagaji.


Anasema yupo tayari kuwekeana kabisa mkataba na mie kwamba gharama zote za mimba na kulea mtoto hatanidai na mtoto ataandikishwa kwa jina lolote nitakalokubali mie na hata akitaka atanilipa. Sijui kaona kitu gani cha ajabu kwa Mnyamwezi mie ingawa kiukweli hadi leo hii sijawahi hata kumbusu, acha kutembea naye.

Kuhusu Mimba anasema inaweza kuwa kwa njia ya kawaida kwa kufanya mapenzi au kwenda hospital na huko wakafanya kupandikiza kama wanavyofanya kwa wale wanaotoa mbegu za Kiume na kuwapa akina mama ambao hata hawawajui.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: