Mpira uko wapi? Fernandinho akimfanyia kitu mbaya James Rodriguez kipindi cha kwanza katika mchezo wa leo mjini Fortaleza.
KATIKA fainali za mwaka 1982 njia pekee ya Italia kumzuia Diego Maradona ilikuwa
ni kumpa jukumu maalum beki wa kati Claudio Gentile ili ale naye sahani moja mwanzo mwisho.
ni kumpa jukumu maalum beki wa kati Claudio Gentile ili ale naye sahani moja mwanzo mwisho.
Gentile alimfanyia faulo 23 Muargentina huyo namba 10 nchini Hispania na Italia walishinda mabao 2-1, huku wakiwaachia wapinzani wao kazi ya kuifunga Brazil katika mechi inayofuata ili wasonge mbele, kitu walichoshindwa kufanya.
Miaka 32 baadaye, kulikuwa na tukio kama hilo kwenye mechi ya Brazil dhidi ya Colombia ambayo imepigwa usiku huu mjini Fortaleza na kushuhudia Fernandinho akipewa jukumu la kumbaka James Rodriguez kwa kila nafasi atakayocheza uwanjani.
Hali tete: Rodriguez akiugulia maumivu baada ya kufanyiwa faulo ya kwanza na Fernandinho, mjini Fortaleza.
Katika dakika ya 14, kiungo huyo wa Manchester City alichuana vikali na Rodriguez katikati ya dimba akijaribu kumpokonya mpira na alimshika nyota huyo wa Monaco.
Mwamuzi alimpa Mcolombia huyo mpira wa adhabu, lakini Fernandinho hakupewa kadi ya njano.
Tayari kulikuwa na maneno kuwa wenyeji wanapendelewa na waamuzi katika mashindano haya, na hili lilikuwa mfano mzuri kwa kuendeleza maneno hayo.
Anaomba: Rodriguez akiomba mpira wa adhabu baada ya kufanyiwa faulo na Fernandinho kipindi cha kwanza.
Kaaah!: Rodriguez akiwa ameanguka chini baada ya kufanyiwa faulo na Fernandinho.
Katika dakika ya 46, Fernandinho alimfanyia faulo Rodriguez.
Rodriguez akionja joto la jiwe kutoka kwa Fernandinho.