April 16, 2014

HII NI KUHUSU MCHUNGAJI ANAYETANGAZA KUWA KANUMBA ALIKUWA FREEMASON, PATCHO MWAMBA ADHAMIRIA KUMSHUGULIKIA..SOMA TAARIFA KAMILI HAPA

  Mwanamuziki na mwigizaji nyota wa muziki wa Dansi Patcho Mwamba  amesikitishwa na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakitafuta thumbnail 1 summary

Patcho Mwamba 
Mwanamuziki na mwigizaji nyota wa muziki wa Dansi Patcho Mwamba  amesikitishwa na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakitafuta
umaarufu kupitia majina ya watu japo kwa kufanya hivyo ni kitu kinachoumiza familia za wanaotendewa hivyo, akitolea mfano kwa mtu anayejiita mchungaji George Kairuki ambaye amekuwa akitumia jina la marehemu Kanumba.

Anatangaza vitu vya uongo eti Kanumba alikuwa Freemason kitu cha uongo kabisa, marehemu Kanumba alikuwa rafiki yangu na mtu wa karibu hakuwa mtu wa ajabu, unaweza kupata kesi kwa mwendawazimu kama huyo,”anasema Patcho.

              Patcho Mwamba, steven Kanumba


Patcho Mwamba anasema kuwa watu kama hawa wanaweza kusababisha matatizo, hata kuua kwa sababu ya ujinga wa watu hao, msanii huyo alisema kuwa anamsikia tu kupitia vyombo vya habari lakini kama siku anajaribu kuongea ujinga huo na yeye akiwepo basi anaweza kufanya kitu kibaya sana ili mtu huyo akome na kuachana na tabia hiyo.

Source:pro-24

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: