Al Shabaab limetoa makataa ya siku kumi na tano kwa wanaotoa huduma za internet kuzifunga. Wanamgambo wa Al Shabaab wenye uhusiano ...
06:22
Al
Shabaab limetoa makataa ya siku kumi na tano kwa wanaotoa huduma za
internet kuzifunga. Wanamgambo wa Al Shabaab wenye uhusiano na Al-Qaeda,
wamesema kuwa wamepiga marufuku raia wanaoishi katika maeneo
wanayodhibiti kutumia internet.
Wapiganaji hao wametoa onyo kwa kampuni zote zinazotoa huduma ya internet siku 15 kufunga biashara zao.
"kampuni yoyote au mtu yeyote
atakayepatikana akipuuza onyo hilo atajulikana kama mtu anayewafanyia
kazi maaduzi zetu, na ataadhibiwa kulingana na sheria za ziisilamu,''
ilisema taarifa ya kundi hilo ambayo ilitumwa kwenye mitandao yake.
Wanamgambo hao hutumia sheria kali za kiisilamu
katika maeneo wanayotawala na kuwakamata watu mara kwa mara kwa tuhuma
za kufanya ujasusi.
Internet hutumiwa sana nchini Somalia, taifa
ambalo limekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa zaidi ya miongo
miwili, huku kundi hilo likionekana kuwa kikwazo kikubwa kwa amani.
Kundi la Al Shabaab zamani lilikuwa likitawala
katika sehemu kubwa za Kusini mwa Somalia na Kati, lakini likaondoa
wapiganaji wake baada ya kushindwa na wanajeshi wa Muungano wa Afrika
wanaopambana nao.
Majeshi ya Afrika ikiwemo wanajeshi kutoka
Uganda, Burundi na Kenya, tangu hapo wamedhibiti sehemu kadhaa kutoka
kwa wapiganaji hao.
Lakini mashambulizi ya kuvizia yanayofanywa na
kundi hilo dhidi ya maslahi ya majeshi ya serikali na yale ya kigeni,
yameondoa matumaini ya kunusuru taifa hilo kutokana na vita vya miaka
mingi.
SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:
No comments
Post a Comment