STAA wa Bongo Fleva, marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ leo anatarajiwa kufanyiwa shughuli ya kumbukumbu ya kifo chake. Habari kutoka ndani ya
familia ya Ngwea zinasema kuwa, shughuli hiyo itafanyika leo Mei 28, nyumbani
kwao Morogoro ikiwa ni mwaka mmoja timilifu tangu afariki dunia.
Staa wa Bongo Fleva, marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’.
Ngwea alifariki dunia Mei 28, mwaka jana katika Hospitali ya St. Hellen jijini Johannesburg, Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu.