Imezoeleka kuwa shindano la Big Brother Africa huwa linaanza mwezi May lakini la mwaka huu 2014 kutokana na kombe la dunia, litaanza September 7 ikiwa
ni season 9 ambapo awamu hii idadi ya nchi zinazoshiriki ni ileile ya nchi 14 ila kuna nchi moja imeondolewa.
Angola wameondolewa na sasa Rwanda
wameingizwa kwa mara ya kwanza huku nchi nyingine zitakazoshiriki zikitajwa kuwa ni Botswana, Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Namibia, Nigeria, Sierra Leone, Rwanda, South Africa, Tanzania, Uganda, Zambia and Zimbabwe.
Washiriki wote ni kuanzia umri wa miaka 21 ambao ni lazima wawe ni Wananchi wa hizo nchi zenyewe na wawe na hati za kusaifiria kutoka nchi hizo.
Tarehe za kuwasaka washiriki wa mwaka huu zitatangazwa mwezi wa sita .