Aliyekua Mgombea wa Urais Ndg. Liberatus Mwang'ombe
2014 hatutambui uongozi mpya ulio tangazwa na Tume ya Uchaguzi jana August 11, 2014. Msimamo wetu ni kuwa; tunapinga matokeo ya uchaguzi ulio fanyika August 9, 2014 kwani ulikuwa sio wa haki na ni BATILI.
“Team Libe for DMV Community President 2014” haitatoa ushirikiano wowote na uongozi wa Jumuia ya Association of Tanzania Community in DMV. Pia tunawaasa wale wapenzi wetu kuto kutoa ushirikiano wowote na uongozi huu batili hadi pale madai yetu
yatakapo sikilizwa na kutatuliwa. Tunaomba wapenzi wetu ambao walijitokeza kupiga kura wawe wavumilivu na watulivu katika kipindi hiki kigumu cha kunyang’anywa haki yao ya kimsingi ya kumchagua kiongozei wanao mtaka.
Mwisho, “Team Libe for DMV Community President 2014” inaitaka “Board of Directors” kutengua uongozi huu uliopatikana kwa njia ya dhulma. Ieleweke kuwa, Team Libe for DMV Community President 2014” na wafuasi wake hatutatoa ushirikiano wowote na uongozi wote wa jumuia.
Fuata hii link kusoma maelezo juu ya ubatili ya huu uchaguzi;
http://libe4dmvpresident2014.blogspot.com/2014/08/tamko-team-libe-for-dmv-community.html
http://libe4dmvpresident2014.blogspot.com/2014/08/mchanganuo-zaidi-kuthibitisha.html
http://libe4dmvpresident2014.blogspot.com/2014/08/team-libe-for-dmv-community-uchaguzi-wa.html
Imetolewa August 12, 2014
Team Libe for DMV Community President 2014
cr: bongoclan