August 13, 2014

WABONGO WAISHIO MAREKANI WAINGIA KATIKA MGOGORO MZITO, KISA NI UCHAGUZI WA VIONGOZI WAO. SOMA HAPA

Aliyekua Mgombea wa Urais Ndg. Liberatus Mwang'ombe Tunapenda kutoa taarifa kwa Umma wa DMV kuwa, Team Libe for DMV Community P... thumbnail 1 summary
Aliyekua Mgombea wa Urais Ndg. Liberatus Mwang'ombe
Tunapenda kutoa taarifa kwa Umma wa DMV kuwa, Team Libe for DMV Community President
2014 hatutambui uongozi mpya ulio tangazwa na Tume ya Uchaguzi jana August 11, 2014. Msimamo wetu ni kuwa; tunapinga matokeo ya uchaguzi ulio fanyika August 9, 2014 kwani ulikuwa sio wa haki na ni BATILI.

“Team Libe for DMV Community President 2014” haitatoa ushirikiano wowote na uongozi wa Jumuia ya Association of Tanzania Community in DMV. Pia tunawaasa wale wapenzi wetu kuto kutoa ushirikiano wowote na uongozi huu batili hadi pale madai yetu
yatakapo sikilizwa na kutatuliwa. Tunaomba wapenzi wetu ambao walijitokeza kupiga kura wawe wavumilivu na watulivu katika kipindi hiki kigumu cha kunyang’anywa haki yao ya kimsingi ya kumchagua kiongozei wanao mtaka.

Mwisho, “Team Libe for DMV Community President 2014” inaitaka “Board of Directors” kutengua uongozi huu uliopatikana kwa njia ya dhulma. Ieleweke kuwa, Team Libe for DMV Community President 2014” na wafuasi wake hatutatoa ushirikiano wowote na uongozi wote wa jumuia.

Fuata hii link kusoma maelezo juu ya ubatili ya huu uchaguzi;
http://libe4dmvpresident2014.blogspot.com/2014/08/tamko-team-libe-for-dmv-community.html
http://libe4dmvpresident2014.blogspot.com/2014/08/mchanganuo-zaidi-kuthibitisha.html
http://libe4dmvpresident2014.blogspot.com/2014/08/team-libe-for-dmv-community-uchaguzi-wa.html

Imetolewa August 12, 2014

Team Libe for DMV Community President 2014

cr: bongoclan

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: