April 25, 2016

Vyeti Feki Vitampa Magufuli Maadui Wengi kuliko Hata "Ufisadi"

Kama kweli Rais Magufuli atahamia katika ukaguzi wa vyeti feki akimaliza ishu ya watumishi hewa ni wazi atapata maadui wengi na idadi yao i... thumbnail 1 summary
Kama kweli Rais Magufuli atahamia katika ukaguzi wa vyeti feki akimaliza ishu ya watumishi hewa ni wazi atapata maadui wengi na idadi yao itakuwa kubwa kuliko anaowapata katika vita yake dhidi ya ubadhirifu.

Watumishi wenye vyeti feki katika utumishi wa umma na makampuni binafsi ni wengi mno. Wengi wao wanafahamika na ndugu zao, marafiki zo na hata majirani zao kwa aidha kufahamu historia zao au kwa kutumia majina tofauti na yale waliyozaliwa nayo au kubatizwa nayo.

Wengi wa watumishi hawa wamepanda ngazi mbalimbali katika utumishi wa umma na hata wengine kufikia ngazi za juu. Wakati mchakato wa vitambulisho vya taifa ulipoanza suala hili linasemekana lilijitokeza kwa kiasi kikubwa katika idara nyeti za serikali lakini kutokana na ukubwa wake ikaamuliwa lifumbiwe macho.

Vyeti feki vinagusa karibu kada zote na katika ngazi mbalimbali mpaka hata zile ngazi zinazoonekana za watu wasioguswa.

Kama Rais JPM akiingia nakugusa huku ni wazi atakuta amegusaa idadi kubwa ya watanzania ikiwemo ile inayomuunga mkono. Tegemezi wa vyeti feki na vyeti feki wenyewe wataendelea kumuunga mkono zamu yao ya kutumbuliwa ikifika? Ndio maana nachele kusema kuwa zoezi la utambuzi wa vyeti feki litamuacha Rais Magufuli na maadui wengi kuliko atakaowapata katika zoezi la ubadhirifu hivyo serikali yake inaweza kupoteza umaarufu ilioanza kuupata. Homa imepanda kiasi kwamba wenye vyeti feki wanaongoza mashambulizi makali ya ukosoaji katika mitandao ya kijamii na popote wapatapo fursa dhidi ya utendaji wa JPM ili kumpunguza nguvu

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW:

No comments