August 23, 2015

MAMA DIAMOND PLATNUMZ AMFUNIKA ZARI KWA MBIZI KWENYE BWAWA

MAMA’KE Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ameonesha umahiri mkubwa wa kuogelea kiasi cha kumfunika mkwe wake, Zarinah Hassan ‘... thumbnail 1 summary
MAMA’KE Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ameonesha umahiri mkubwa wa kuogelea kiasi cha kumfunika mkwe wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwenye bwawa la kuogelea lililopo nyumbani kwa Diamond, Tegeta-Mivumoni jijini Dar.

Mama huyo alionekana akipiga mbizi na mtoto wake Esma, huku akionyesha manjonjo ya kuogelea kwa kasi tofauti na Zari anavyoogelea katika bwawa hilo.

“Bi mkubwa yuko vizuri sasa maana anapiga mbizi siyo mchezo kabisa hata Zari haoni ndani, spidi yake ni kali kuliko Zari,” alisema mwanafamilia mmoja ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini huku akimtumia mwandishi wetu picha za mama Diamond akiogelea.

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: