Kuna msemo usemao mtoto wa nyoka ni nyoka, na hii inaweza kujidhihirisha kwa mtoto wa mwanasoka bora wa ligi kuu ya England Wyne Rooney aitwaye Kai.
Rooney ana watoto wawili Kai na Klay ambao ni kama wanafuata nyayo za baba yao kutokana na kuanza kuonyesha kipaji wakiwa bado wadogo.
Kai aliamua kuungana na baba yake jana ndani ya uwanja mara baada ya pambano kati yaManchester United na Arsenal mchezo ambao walitoka sare ya 1-1.