Kosa: Blerim Dzemaili shuti lake lilipita mikononi mwa kipa Claudio Bravo jana usiku.KOSA binafsi la kipa wa Barcelona, Claudio Bravo katika mechi yake
ya kwanza liliwapa Napoli ushindi wa bao 1-0.
ya kwanza liliwapa Napoli ushindi wa bao 1-0.
Kiungo wa Napoli, Blerim Džemaili aliweza kufunga bao hilo pekee la ushindi mjini Geneva.
Kipa huyo raia wa Chile alicheza vizuri mpaka aliposhindwa kudaka shuti la mbali zikiwa zimesalia dakika 10 tu mpira kumalizika na kuwapa ushindi vijana wa Rafa Benitez dhidi ya Luis Enrique.
Barcelona bado wanaendelea kuwakosa washambuliaji watatu chaguo la kwanza, Leo Messi, Neymar na Luis Suarez na jana walishindwa kufunga mabao mpaka Bravo akawapa faida wapinzani.
Kaaah! nimechemka!: Kipa wa Chile aliishia kuutazama mpira unaozama nyavuni mjini Geneva
Blerim Dzemaili hakuweza kuamini bahati yake baada ya kufunga goli hilo.
Hapa majanga tu: Bosi mpya wa Luis Enrique alishangaa kuona vijana wake wanapigwa kidude.