July 31, 2014

“Arsenal haikuwa na hadhi ya kumsajili Suarez.” – mtambue aliyesema kauli hii

Wakati wa dirisha la usajili msimu uliopita mchezaji Luis Suarez alitingisha vichwa vya habri vya vyombo vya habari zote kutokana na ku... thumbnail 1 summary
BPKfv3-CMAAcsY9.jpg-large
Wakati wa dirisha la usajili msimu uliopita mchezaji Luis Suarez alitingisha vichwa vya habri vya vyombo vya habari zote kutokana na kuwania na vilabu vingi vikitaka kumsajili kutoka Liverpool.

Klabu bingwa ya FA Cup Arsenal ilikuwa ni moja ya timu iliyokaribia kabisa kumsaini mshambuliaji huyo wa Uruguay baada ya kutuma ofa ya £40 na senti moja, ofa ambayo ilikuwa imefikia kiasi ambacho Liverpool walikiweka kwenye mkataba ikiwa timu yoyote itahitaji kumsaini Suarez, hata hivyo uhamisho huo ulishindikana na Suarez akabaki Liverpool.
Takribani miezi 12 imeshapita sasa tangu uhamisho huo ushindikane na Suarez tayari ameshaenda FC Barcelona kwa ada ya uhamisho wa £75, na kuondoka kwake Liverpool kumeacha majonzi makubwa Anfield, huku nahodha wa klabu hiyo
Steven Gerrard akikiri kuhuzunishwa mno na kuondoka kwa Suarez.
Pamoja na kukiri kuhuzunishwa na kuhama kwa Luis Suarez, Gerrard pia amezungumzia sakata la uhamisho wa Suarez uliofeli kwenda Gunners.
Gerrard anasema: “Ningeumia zaidi na kuhuzunishwa kumuona Luis akihamia Arsenal. Pamoja na heshima  nilizonayo kwa Arsenal, nilimwambia kwamba kwa kiwango chake kikubwa hakustahili kuichezea Arsenal. Nilimwambia kama utaendelea kuwa nasi, ukafunga mabao 30 basi utashinda uchezaji bora wa ligi pamoja na tuzo ya mchezaji bora wa chama cha waandishi wa habari – na hapo ndipo Real au Barcelona zitakufuata kukusajili. Nadhani watu wengine wa karibu walimshauri vibaya msimu uliopita, wakimwambia anahitaji kucheza
kwenye champions league bila kujali kwenye timu gani.”
Nahodha huyo wa Liverpool aliendelea kusema kwamba kama mshambuliaji huyo angeendelea kubaki Liverpool msimu huu, basi klabu yao ingekuwa na nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa: “Naamini kama tungekuwa na Suarez basi tungekuwa na nafasi zaidi. Nina majonzi kuona ameondoka lakini nina furaha kwa ajili yake kwa sababu amepata alichotaka na anachostahili.”

SHARE THIS POST TO SOCIAL MEDIA BELOW: